Listening to General Secretary Bankmoon addressing delegates from different countries on the theme of session

Having a lunch with other delegates from different countries day one at UN Geneva-Switzerland(Europe)

The storm ended in 2012. It was the day unspeakable, and the joy unforgettable at Chimwaga Hill Conference: The University of Dodoma-UDOM

With special attention while taking photos at American Embassy in Nairobi Kenya

With the smiling face in Nairobi Kenya at American Embassy :From the left is Dannilo from Mozambique, Anderson from Tanzania, Dr.Katabaro-Tz, and the blogger in the right side Dr.Msoline

Saturday, 27 February 2016

HONGERA SANA KAKA VICTOR J. MSHANA


HONGERA SANA KAKA VICTOR J. MSHANA
 
Iliwashangaza wengi pale kaka yetu Victor Mshana alipotangaza kuwa amepata mchumba. Wengi walifurahia sana. Lakini iliwashangaza wengi wengi pale alopseama anataka kuoa rasmi.

Basi, maamuzi aliyoyachiukua Victor yalipongezwa sana hasa marafiki zake na familia kwa ujumla pale Victor aliptamka rasmi kwa baba yake mzee Msahana…..’’Baba, nimepata mchumba, na kwa umri huu nataka niachanae na ukapera na niwe na familia yangu niishi kama mme na mke….’’

Baba akakubali maana imeandikwa …Mtoto atamwacha baba na mama yake, na ataambatana na mkewe na kuishi kama mke na mme.

Ndipo tarehe 20.02.2016 ilikuwa siku ya kipekee kwa kaka yangu Victor Mshana alipoudhihilishia ulimwengu kuwa yeye na ukapera BYE! BYE!


Ni siku hiyo Victor bila kupepesa macho wala kuogopa aliyatamuka maneno haya mbele ya waumini na mbele ya mchungaji….’Mimi Victor Mshana, nakubali kumuoa  …………..ili awe mke wangu wa ndoa, nitaishi nae katika shida na raha, ugonjwa na afya, utajili na umasikini….. hadi kifo kitutenganishe.

Uriiiiiiiiii, Uriiiiiiii, Uriiiiiiii……. Ni sauti za vigeregere zilizosikika kutoka kwa waumini pale Victor alipoitumbukiza pete kwenye kidole cha bi harusi na bi harusi naye akaitumbiukiza pete kwenye kidole cha Bwana harusi ambae ni Victor

 
Baada ya ndoa kanisani, tukio lilifouta nyuma lilikuwa la kipekee, vijana wakajimwaga kuchukua picha za matukio.

Ni katika sanamu ya mnyama aina ya Faru, kama sehemu ya wanyama waa kitalii nchini Tanzania, basi bwana na bibi wakasema tukachuke picha hapa kwenye sanamu ya mnyama huyu

Ni katika jengo la ghorofa ya 16 jengo lefu sana, basi bwana na bibi wakasema kwanza tupande huko juu ili tuone chini panaonekaje. Chini wakaona uwanda mzuri wa Tanzania mjini Arusha, ukingaa nao wakafurahia upepo mzuri na mwanana
Ni katika uso wenye furaha katika bustani iliyoandaliwa mahususi kwa hawa wawili, yaani Mr and Mrs
Mrs akaamua kumbeba mgongoni Mr. Mbereko ndiyo ilikosekana, lakni Mr alibebwa kama ujuavyo......


...Nyanyuka mama, wewe ndo kila kitu, nimekusotea mda mrefu (Mr akimwambia Mrs)

Maakuli hayo nyuma ya bwana na bibi harusi. Ndafu ilikuwepo, pilau, wali mweupe, kachumbali. Watu walikula haoo, wakanywa, wakacheza, sema ni wewe tu uliyekosa, lakini tukio lilifana kweli

Vijana wenzake bwana harusi wakimjoki kwa nyuma, wakimkumbusha ya nyuma hadi bwana na bi harusi wakashtukia washaangua kicheko. Mambo ya vijana hayo.

 Ilikuwa ni siku ya kipekee kwa kaka Victor Mshana. Kwa niaba nzima ya vijana wenzako, tukutakie maisha yenye baraka na amani. kwa zawadi ya kipekee, tunakuzawadia biblia ewe Bwana harusi, soma sana biblia, umo ndo kuna maarifa ya jinsi ya kumtunza mkeo na kuitunza famila. N a kwako Bi harusi, tunakuzawadia kitabu cha Tumwabudu Mungu Wetu, imba sana, mmeo hata akiwa mkorofi kiasi gani, wewe imba tu.

0 comments:

Post a Comment