Listening to General Secretary Bankmoon addressing delegates from different countries on the theme of session

Having a lunch with other delegates from different countries day one at UN Geneva-Switzerland(Europe)

The storm ended in 2012. It was the day unspeakable, and the joy unforgettable at Chimwaga Hill Conference: The University of Dodoma-UDOM

With special attention while taking photos at American Embassy in Nairobi Kenya

With the smiling face in Nairobi Kenya at American Embassy :From the left is Dannilo from Mozambique, Anderson from Tanzania, Dr.Katabaro-Tz, and the blogger in the right side Dr.Msoline

Wednesday, 3 December 2014

HUKUMU IMETOLEWA. JE, TUNAJIFUNZA NINI KUTOKANA NA MSICHANA WA KAZI (MIAKA 22) KUMTESA MTOTO WA MIEZI 18?



HUKUMU IMETOLEWA. JE, TUNAJIFUNZA NINI KUTOKANA NA MSICHANA WA KAZI (MIAKA 22) KUMTESA MTOTO WA MIEZI 18?

Katika mwezi wa 11 mwaka huu wa 2014, mitandao yote ya kijamii na vyombo vyote vya habari viliandika juu ya binti wa kazi huko nchini Uganda kumtesa mtoto mchanaga wa miezi 18. Wengi walilaani kitendo cha huyu binti alichokifanya kwa mtoto mchanga. Na zaidi wengi walisema ahukumiwe kifungo cha maisha jera au auawe kwa unyama alioufanya.

Ilikuja kugundulika baada ya mwenye nyumba(baba wa mtoto) kuona kwenye kamera ya ulinzi iliyofungwa kwenye nyumba yake, ndipo akampa kichapo binti wa kazi na binti akaamua kukimbilia polisi, baba mwenye nyumba alipokamatwa akaelezea kisa cha kumpga binti huyo na video akaitoa kama ushahidi. Ndipo kibao kikamgeukia binti wa kazi na kuwekwa rumande akisubilia hukumu ya kutaka kuua kwa kukusudia.

Wiki moja baadae nilishangaa kukuta katika chombo kimoja cha kimataifa kimeandika kuwa Saudi Arabia imekataza raia wake kuajili Mayaya(wasichana wa kazi toka Uganda) kulingana na kitendo cha binti wa kazi wa Kiganda alichomfanyia mtoto mchanga. Mara hii jamani? Kosa amefanya mtu mmoja lakini jamii nzima ya Uganda imehukumiwa (Do not generalize)

Ni sawa binti wa kazi alikuwa na kesi ya kujibu ambayo iko wazi kwa kila mtu na ushahidi ukiwa unajionesha waziwazi bila chenga. Na wengi wao walitoa hukumu zao, wengine wakisema afungwe maisha jera, wengine wakitaka auawe. Ilimradi kila mwenye mdomo alisema kilicho chake na weye uwezo wa kuandika waliandika kama walivyoona.

Ni ukweli usiopingika kuwa binti alifanya kosa, na kosa kubwa, na Madakitari walimpima na kukuta ana akili timamu lakini kuna binadamu yeyote ambaye amejiuliza walau maswali mawili juu ya huyo binti?
Tunaposoma biblia tunaona Mwenyezi Mungu alituumba wanadamu wote tukiwa wakamilifu, na tukirudi kwa upande mwingine(Sociological Analysis) tunaona kuwa baada ya kufika duniani, mwandadamu anakutana na mazingira mapya, watu wapya na mengine mengine ambayo yanamzunguka na kufanya ukamilifu wake upotee na kuwa mpya katika mazingira yanayomzunguka (socialization)

Nikirudi pale pale kwa binti wa kazi na kitendo chake alichokifanya, ni kweli ni kosa kubwa na nazidi kusema ni kosa kubwa sana, lakini hatukupaswa kumhukumu haraka sana kwa kitendo chake alichokifanya na uthibitisho wa madakitari kuwa ni mzima wa akili. Tunapaswa kuangalia historia ya binti huyu, na familia anayotoka. Kiubinadamu,huenda kuna jambo lilimuumiza huko nyuma, nayeye bila kujua hasira akazimalizaia kwa mtoto mchanga(tena bila kujua kuwa anafanya makosa). Ni wengi sana tumeshuhudia wapenzi wakisalitiana na wengine wanachukua maamuzi ya gafla mfano kupasua kitu, kuchana nguo au hata kujiua. Haya yote ni historia ya kitu fulani na mwishowe wengine hujutia. Ndivyo ilivyo kwa huyu dada wa kazi.

Mimi nadhani pamoja na hukumu yake ya kutaka kuua kwa kukusudia, pia ningependa wanasociologia na wanasaikolojia wangeongea na huyu binti ili kujua behind the incidence kuna nini. Najua kuna kitu nyuma ya pazia kimejificha.

Yametokea hayo na tunamshukuru Mungu mtoto mwenyewe hajafa, amepona majeraha na ni mzima wa afya. Je, wazazi tunajifunza nini kutokana na hili lililotokea? Waswahili wanasema leo kwangu, kesho kwako. Kama huyu mtoto amejeruhiwa vibaya, jua wa kwako ndo utamkuta kabanikwa kwenye moto.

Ni vizuri wazazi kama munataka kuleta wasaidizi wa kazi kuweni makini nao, walau kwa kujua historia ya maisha yao, na familia wanakotoka. Pia wazazi ishi na wadada wa kazi vizuri kwani wengi wao wanateswa na waajili wao hivyo wanaamua kulipiza kisasi kwa hayo wanayotendewa.
Pamoja na hiyo, kama mna mtoto mchanga na nyie wazazi nyote ni waajiliwa ni vizuri mkawa na utaratibu mzuri wa kulea mtoto wenu kama kuomba ruhusa ya kufanya kazi za ofisi ukiwa nyumbani kwako huku ukilea mtoto wako, au kumpeleka mtoto kwenye vituo vinanyoaminika vya kulea watoto wadogo(day care centre), au kuajili bibi wa mtoto kulea mjuu wake.
  
Asanteni sana na siku njema.

0 comments:

Post a Comment