Listening to General Secretary Bankmoon addressing delegates from different countries on the theme of session

Having a lunch with other delegates from different countries day one at UN Geneva-Switzerland(Europe)

The storm ended in 2012. It was the day unspeakable, and the joy unforgettable at Chimwaga Hill Conference: The University of Dodoma-UDOM

With special attention while taking photos at American Embassy in Nairobi Kenya

With the smiling face in Nairobi Kenya at American Embassy :From the left is Dannilo from Mozambique, Anderson from Tanzania, Dr.Katabaro-Tz, and the blogger in the right side Dr.Msoline

Thursday, 27 October 2016

ZAO LA MUHOGO


LIFAHAMU ZAO LA MUHOGO
UTANGULIZI
Muhogo(manica esculentum) ni zao la jamii ya mizizi kama vile viazi, linalostawi vizuri katika maeneo yaliyopo kwenye mwinuko wa mita 0-1500 toka usawa wa bahari. Zao hili hustawi kwenye maeneo yanayopata mvua za wastani wa 750mm hadi 1200mm kwa mwaka, hustawi vizuri kwenye ardhi yenye udongo wa Kichanga usiotuamisha maji.
Mihogo ni zao muhimu sana kwa Tanzania kutokana na sifa zake za kuvumilia ukame, kustawi kwenye maeneo yenye rutuba kidogo, hivyo inahitaji gharama ndogo za uzalishaji.
Kwa hali hiyo zao za Muhogo linaweza kulimwa zaidi na wakulima wadogo wadogo wenye vipato vidogo huko vijijini.

AINA ZA MIHOGO
Nchini Tanzania, kuna aina zaidi ya 45 za Mihogo na zaidi ya 80% ya mihogo hii ni ya asili(Kituo cha utafiti wa mazao ya Kilimo-Naliendele). Hii ina maana kuwa wakulima wengi wanalima mihogo ya asili.
Mihogo michungu bado inaendelea kulimwa kwenye jamii zetu kwa sababu haishambuliwi kirahisi na magonjwa na wadudu, ila pia ni rahisi kuhifadhi baada ya Mavuno.
a.     MIHOGO YA ASILI
Mihogo ya asili ni ile iliyolimwa miaka mingi iliyopita na kurithiwa vizazi kwa vizazi. Mihogo hii ina sifa zifuatazo:-
·        Hutoa mavuno wastani wa Tani 10 hadi 20 kwa hekta.
·        Inaweza kuhifadhiwa shambani kwa mda mrefu bila kuoza.
·        Huchukua muda mrefu kukomaa(kufikia hatua ya kuvunwa)
·        Hushambuliwa kirahisi na magomnjwa kama Michrizi ya kahawia, batobato na blaiti
·        Hushambuliwa na wadudu aina ya millibagi
·        Wakulima wanaijua vizuri , tabia na utunzaji wake.

b.     MIHOGO BORA
Hii ni mihogo iliyofanyiwa utafiti na wataalamu na kuthibitishwa na Kamati ya Mbegu ya Taifa kufaa kwa matumizi ya wakulima. Kupitia kituo cha utafiti wa mazo ya kilimo cha Naliendele, Mtwara mbegu aina ya Naliendele na Kiroba zilifanyiwa utafiti kukubalika kutumiwa na wakulima wa Mihogo nchini Tanzania.
Sifa za mbegu hizi ni zifuatazo;-
·        Hutoa mavuno ya Tani 19-30 kwa hekta.
·        Hustahimili mashambulizi ya magonjwa kama vile Michirizi ya Kahawia, Batobato na Blaiti.
·        Hukomaa kwa kipindi cha Miezi 9 baada ya kupanda.

MAGONJWA NA WADUDU WAHARIBIFU KWA ZAO LA MUHOGO
Zao la muhogo linashambuliwa na magonjwa makuu mawaili ambayo ni Michrizi ya kahawia/Matekenya na Batobato/ukoma wa majani(cassava mosaic disease), na wadudu waharibifu kwa zao la Muhogo ni kama wafuatao: Cassava Mealy Bug(CMB), Cassava Green Mites(CGM), White Scales na Mchwa.
Pia, wanyama wanaharibu sana mazao ya Mihogo yakiwa shambani, wanyama hawa ni kama vile: Nguruwe na Panya.
Magonjwa haya ya zao la mihogo yanasababishwa na virusi(ipomovirus) na kuenezwa kutoka mmea mmoja na mwinginge kupitia Nzi Mweupe(white fly) na mdudu aina ya Bemisia afer. Sehemu za mmea ambazo hushambuliwa na magonjwa haya ni pamoja na Majani, Shina na Mizizi kulingana na hatua ya ukuaji wa muhogo.
Dalili zake kulingana na magonjwa niliyoyataja hapo juu ni kama zifuatazo: Rangi ya njano kwenye majani, rangi ya dhambarau/kahawaia kwenye shina, kufa kwa mizizi ya muhogo, ukuaji usiolingana wa majani, kujikunja na kupungua umbo kwa majani, kudumaa kwa mmea na majani machanga kuvimba.

JINSI YA KUZUIA NA KUDHIBITI MAGONJWA NA WADUDU WAHARIBIFU
·        Kuchagua mbegu kutoka mmimea isiyo na dalili za ugonjwa.
·        Hakikisha unapanda mbegu bora za muhogo zinazostahimili uambukizo wa Magonjwa.
·        Kuelewa dalili za magonjwa kwa ajili ya kuchukua hatua haraka.
·        Kutunza mbegu bora zinazovumilia magonjwa sana.
·        Kuweka shamba safi kupunguza visababishi vya magonjwa.
·        Kutumia dawa za kuulia wadudu waharibifu.
·        Hakikisha unateketeza mihogo iliyo athirika baada ya mavuno.

UVUNAJI NA USINDIKAJI WA MUHOGO
Mihogo inaweza kuanza kuvunwa baada ya miezi 9 hadi 12 tangu kupandwa. Inashauriwa kuvunwa katika kipindi cha Jua kwasababu ukivuna kipindi cha mvua kiwango cha wanga hupungua.
Usindikaji bora wa muhogo unafanywa kwa sababu zifuatazo: Kurahisisha/kuharakisha ukaushaji, Kuondoa sumu(cynanide) iliyoko kwenye baadhi ya aina za mihogo na Kuongeza thamani(value addition) zao la muhogo kwa kutengeneza unga wa muhogo.




Njia bora za usindikaji wa Muhogo
a.     Kwa kutumia mashine aina ya Grater
Hii hutoa chembechemebe laini za muhogo amabazoz baadae hukamuliwa kwa kutumia kifaa kiitwacho “presser” ili kuondoa sumu iliyoko kwenye muhogo. Hii mashine ni mahususi kwa muhogo mchungu.
b.     Kwa kutumia mashine ya chipper
Mashine hii hutoa vipande vidogo vidogo(chips) na hutumika hasa kwa ajili ya mihogo mitamu/baridi.

MATUMIZI YA MUHOGO
·        Muhogo unaweza kupikwa wenyewe kama chakula au kutengeneza unga
·        Unga wa muhogo unaweza kutumika kutengeneza vitu vyote vinvyotengenezwa na unga wa ngano kama vile: Biskuti, chapatti, maandazi, chichili, keki n.k
·        Pia, muhogo unaweza kutumika viwandani kutengeneza bidhaa zingine kama vile Wanga.




                        Imeandaliwa na Mtaalamu wa Uchumi Kilimo na Biashara
                        SAMSON ALFRED SHILA
                        MTWARA-MANISPAA

0 comments:

Post a Comment