Zifuatazo ni njaa mbili zinazowasumbua wanandoa endapo hawatashibishana.
1. Njaa ya mwanamke ni upendo:
Mwanamke anahitaji upendo kuliko vitu vingine, hata katika vitabu vya
dini vinasema; enyi waume, wapendeni wake zenu. Ampendaye mkewe
hujipenda mwenyewe, mwanaume anatakiwa kujitoa kwelikweli kumpenda mke
wake kama tunavyojua upendo ndio falsafa kubwa sana katika maisha ya
binadamu, upendo huvumilia, hufadhili, hauhusudu. Hivyo basi njaa ya
mwanamke ni kupendwa. Wewe kama mwanaume unatakiwa kumpenda mke wako kwa
moyo wako wote bila kujali udhaifu wake. Hii ndio njaa ya wanawake
wanahitaji upendo katika maisha ya ndoa.
2. Njaa ya mwanaume ni kuheshimiwa:
Mwanaume njaa yake kubwa ni kuheshimiwa katika maisha ya ndoa. Sasa ikitokea mwanaume anakosa kuheshimiwa na mke wake katika maisha ya ndoa hivyo anakuwa amekosa kushibishwa njaa yake. Na kama akikosa kushiba ndio matatizo huanzia hapo itamlazimu kutafuta kushibishwa njaa yake nje. Hivyo kama wewe ni mwanamke unatakiwa kumshibisha mume wako njaa yake ya kumtii.
Kama wanandoa wanashindwa kushibishana njaa zao, hivyo wanajitengenezea shimo wao wenyewe. Watu wanajisahau sana katika kutimiza majukumu yao katika maisha ya ndoa hatimaye wanaruhusu haki za kibinadamu kuingia maisha ya ndoa, kama wanandoa mkishaingiza haki za kibinadamu katika maisha ya ndoa yaani hamsini kwa hamsini kama wanavyodai lazima mtapoteza mwelekeo tu.
Kwa hiyo kila mtu ana njaa yake kama tulivyoona hapo juu sasa mkishayaingiza mambo haya ya kidunia mtakosa kushibishana njaa zenu.
Mwisho, kila mwanandoa ana wajibu wa kumshibisha mwenza wake, mke akipendwa atashiba njaa yake na mume akiheshimiwa atashiba njaa yake. Kila mtu ana njaa yake hivyo mnatakiwa kushibishana na kupendana katika shida na raha.
2. Njaa ya mwanaume ni kuheshimiwa:
Mwanaume njaa yake kubwa ni kuheshimiwa katika maisha ya ndoa. Sasa ikitokea mwanaume anakosa kuheshimiwa na mke wake katika maisha ya ndoa hivyo anakuwa amekosa kushibishwa njaa yake. Na kama akikosa kushiba ndio matatizo huanzia hapo itamlazimu kutafuta kushibishwa njaa yake nje. Hivyo kama wewe ni mwanamke unatakiwa kumshibisha mume wako njaa yake ya kumtii.
Kama wanandoa wanashindwa kushibishana njaa zao, hivyo wanajitengenezea shimo wao wenyewe. Watu wanajisahau sana katika kutimiza majukumu yao katika maisha ya ndoa hatimaye wanaruhusu haki za kibinadamu kuingia maisha ya ndoa, kama wanandoa mkishaingiza haki za kibinadamu katika maisha ya ndoa yaani hamsini kwa hamsini kama wanavyodai lazima mtapoteza mwelekeo tu.
Kwa hiyo kila mtu ana njaa yake kama tulivyoona hapo juu sasa mkishayaingiza mambo haya ya kidunia mtakosa kushibishana njaa zenu.
Mwisho, kila mwanandoa ana wajibu wa kumshibisha mwenza wake, mke akipendwa atashiba njaa yake na mume akiheshimiwa atashiba njaa yake. Kila mtu ana njaa yake hivyo mnatakiwa kushibishana na kupendana katika shida na raha.





0 comments:
Post a Comment